Latest Updates

HIZI NDIO SABABU ZA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED KUTAKA MOYES ATIMULIWE

West Brom wameshinda Old Trafford msimu huu baada ya miaka 35...Everton baada ya miaka 21 na Newcastle baada ya miaka 41...YOTE HAYA YAMETOKEA BAADA YA FERGIE KUSTAAFU NA KUMKABIDHI MOYES TIMU.



HAYA NDIO MAONI YA MASHABIKI:
 
Kweli kuna tofauti kubwa sana kati ya Sir Alex Ferguson na David Moyes.

Lakini ukiangalia kwa jicho la tatu, nakubaliana na kauli ya Moyes kwamba anahitaji kupata wachezaji wa kiwango cha dunia angalau hata watano.

Mpaka kufikia hapa kamjaribu kila mchezaji. Zaha ni kichekesho, sio wa kubadilisha matokeo, Januzaj bado anatakiwa aendelee kuchezea U21 pengine kajisahau.

Wachezaji wanaonyesha kiwango duni sana, tutaendelea kuwalilia baadhi ya wachezaji kwamba hampangi fulani na fulani tutaanza na Fletcher sasa.

Moyes apewe fungu asajili wachezaji anaotaka hapo januari kisha tuje tumbebeshe lawama vizuri.

Lakini kwa wachezaji hawa wasiojituma tutaendelea kuporomoka zaidi.

Shukurani zangu ni kwa Wayne Rooney ambae amekuwa mpiganaji wakati wote, tumuongezee wachezaji watatu au wanne wenye moyo wa upiganaji kama yeye watatusaidia.