King wa swagga za TAKEU Afrika Mashariki aliye the big boss wa Bush Band, Nice Lucas Mkenda ‘Mr Nice’ amejibu mapigo kwa ‘kuwavua nguo’ waliokuwa wapenzi wake, mcheza filamu Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ na msichana wa mjini, Lulu John, Amani linakupasha.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu ya kiganjani akiwa kwenye kampeni za CCM Kahama, Shinyanga, Nice aliwachana vibaya warembo hao na kudai kuwa hajawahi kuanguka nao dhambini kama wenyewe wanavyobandika mabango jijini Dar.

Mr Nice akiwa na Jini Kabula.
Huku
akiwahusisha warembo hao na skendo mbaya ya uchangudoa, Nice aliwaruka
vibaya huku akidai jambo linalomkera zaidi ni kitendo cha Kabula na Lulu
kujipakazia kuwa yeye ni mume wao.Nice aliendelea kuwapaka ile mbaya wasichana hao wanajiita watoto wa mjini huku akidai kuwa hafanani na sampuli yao hata tone.
“Wamechanganyikiwa na maisha, mtu huwezi kuitwa Jini, kwanza nawashangaa sana kwasababu siwatambui, wasitake kutafuta umaarufu kupitia kwangu,” alisema Nice anayejiandaa kwenda nchini Norway katika mwaliko wa kikazi.

Lulu John.
Amani
lilimtafuta Jini Kabula na kumsomea ‘eituzedi’ ya aliyotoa Nice ambapo
alikuwa na haya ya kusema: “Hawezi kututukana sisi wakati tumemfuga hapa
mjini, hana lolote sisi hatuwezi kujipendekeza kwake, suala la
uchangudoa, hatujawahi kujihusisha na ufuska huo.”