Latest Updates

BINT AUWAWA KIKATILI SENGEREMA NA KUTUPWA MAENEO YA MAKABURI !!





Askari kanzu waliofika eneo la makaburi ambapo bint
huyo aliuwa kinyama na watu wasifahamika Kumradhi kwa picha hizi



Askari akiangalia kwa makini mwili wa dada huyu ambaye ameuwa kikatili na watu wasifahamika








hee mwenyezi mungu ilaze roho ya huyu dada peponi


Bint moja kakutwa kauwawa maeneo ya mkaburi ya kata ya nyatukala na maiti yake kuwachwa pembezoni mwa kaburi.


Akitoa tarifa mtendaji wa kata nyatukala.ambaye pia ni Diwani mh Adamu akisimulia mkasa huo hali halisi juu ya mkasa huu.


Akifafanua zaidi mh adamu alisema kuwa baada ya kuona hali hiyo walibidi wafanya masiliano na jeshi la polisi ili wawenze kuja eneo hilo la tukio.
Aidha baada ya kufika Askari hao eneo la tukio hilo na kuona mwili huo waligundua katika mwili wake marehemu alipingwa na kitu kizito nyuma ya kisongo chake kichwani na maeneo ya mabenga yake .


Mh Adamu alizidi kusema kuwa kutokana na hali hiyo ya kuvuja damu nyingi ndiko kumesababishwa Bint huyo kukutwa na mauti hayo .
Aidha Mtendaji huyo amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni bado ni kitendawili katika kata hii na kusema kuwa chazo cha tukio hili halisi ni bado na jeshi la polisi enaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.