Latest Updates

Unajua muda ambao ‘Mwana’ ya Ali Kiba imekaa studio kabla ya kutoka..? Ya Mr. Blue je?


Inawezekana ukubwa wa singo kadhaa ambazo zimewahi kuhit zinatokana na uvumilivu wa baadhi ya watayarishaji wa kazi hizo za muziki (producers), millardayo.com imepata nafasi ya kuongea na Man Walter ambaye ni mmiliki na producer wa studio ya Combination Sound, iliyopo Kinondon Dar.

Man Walter kazungumzia hili; ‘Mimi mara nyingi ngoma ambazo zimekaa muda mrefu na kuchelewa kutoka ni pamoja na ‘Mwana’ ya Ali Kiba umekaa miaka 4 studio.. wimbo mwingine ni wa Mr.Blue ‘Nipende Kama Nilivyo huu ulikaa miaka 5‘

‘Kwa wakati mwingine msanii anaweza asishtukie kama huu wimbo ni mkali tunaweza tukaanza idea tukaicha, tukarukia zingine zikaendelea kutoka lakini baadaye mi’ sikio linarudi kwenye kile tulichokianza wakati huo miaka ishaenda, ninapokifurumua inakua issue sasa yeye msanii kwake anaona kitu kipya‘

‘Tunapopata kitu kipya kwa wakati huo inabidi tukumbuke tulianza lini na ndipo tunapoanza kujumlisha miaka tunapata miaka mingi zaidi‘.