Latest Updates

HAWA NDIO MAWAZIRI WALIOJIUZU NA SABABU ZAO

BAADA ya Waziri wa Maliasili na Utanii Balozi Khamis Kaghasheki kujiuzuru, Waziri Mkuu Mizengo Pinda pia alifikia hatua ya kujiuzuru kwa staili ya kusubiri uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete, ambaye yuko nchini Marekani kwa uchunguzi wa Afya yake, hatua ya mawaziri kuwajibika inatokana na vitendo vya mauaji ya wananchi na mifugo yao pamoja na manyanyaso makubwa, zilizofanywa na Wanajeshi wa Tanzania wakati wa Operesheni Tokomeza Ujangili, kwakuwa yeye ndiye msimamizi wa shughuli zote za serikali.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kulia),(kushoto) Askari wa Jeshi la Polisi ikitekeleza majuku yao
Mbali na Waziri Mkuu mawaziri wengine waliokumbwa na kashfa hiyo na kulazimishwa kujiuzuru ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani na nchi (Dk Emmanuel Nchimbi), Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (Shamsi Vuai Nohodha)na Waziri wa Uvuvi na Mifugo (Mathayo David Mathayo).
"Nimezungumza na mawaziri,nimezungumza na mkuu wa nchi, kuhusu hali ilivyo nchini,mawaziri wamekubali kuwajibika na Rais Kikwete amebariki uamuzi wao"alisema Pinda.