Latest Updates
Home »
Uncategories »
KELLY ROWLAND AKIWA UWANJA WA FISI MANZESE
KELLY ROWLAND AKIWA UWANJA WA FISI MANZESE
Msanii maarufu wa Marekani Kelly Rowland, ametinga uwanja wa fisi Manzese Dar es salaam jana jioni baada ya kusikia sifa za maeneo hayo ya
Uswahilini
tangu akiwa USA. Msanii huyo ametua nchini kwa tiketi ya MTV kupitia
taasisi yake inayojishughulisha na kampeni za kupambana na Ukwimwi (Staying Alive Foundation)
ya nchini Marekani, Kelly akiwa balozi wake. Akiwa Uwanja wa Fisi,
ambako kunasifika kwa ufuska wa kupindukia na rate kubwa ya maambukizi
ya virusi vya ukimwi kwa wasichana wadogo, Kelly alitembelea NGO ya EYG
(Elizabeth Youth Group) inayojishughulisha na kutoa misaada ya elimu ya
HIV/AIDS, uchangudoa, ulevi pamoja na uvutaji bangi kwa vijana nchini.

