Latest Updates

WANAWAKE KUMBE NAO WAMO...MKE AWAMWAGIIA MAJI YA MOTO MUME NA MWANAE


Bw. William Mushi (32), aliyemwagiwa maji ya moto na mke wake, Tunu Kimaro.
NI HALI YA KUSIKITISHA NA KUSTAAJABU KWA JAMII BAADA YA TUNU KIMARO KUMMWAGIA MAJI YA MOTO MUMEWE, WILLIAM MUSHI (32), MKAZI WA MABIBO JIJINI DAR ES SALAAM PAMOJA NA MTOTO WAKE MCHANGA.
Tukio hilo la kikatili lilitokea Agosti 15, mwaka huu nyumbani kwake Mabibo jijini Dar es Salaam na lilishangaza majirani kutokana na Tunu kudaiwa kuchukuwa maji ya moto yaliyokuwa yanachemka na kuwamwagia bila huruma.
CHANZO NI MTOTO
Akisumulia mkasa huo Mushi alikuwa na haya ya kusema:
“Mke wangu anaitwa Tunu Kimaro ana miaka 23. Alinimwagia maji ya moto baada ya kumkuta mwanangu wa miezi saba hali yake ya kiafya ikiwa siyo nzuri, nilipokuwa naondoka asubuhi nilimuagiza ampeleke hospitali.


Mtoto mchanga wa Bw.William Mushi aliyeunguzwa pia na maji ya moto.
“Baada ya kufika nyumbani na kumkuta mwanagu Ivan amenyong’onyea, nilipomuuliza mke wangu sababu za kutompeleka hospitali alinijibu majibu ya kijeuri kama siyo mke wangu na mtoto siyo wake.
“Niliendelea kumtaka anieleze sababu ya kutompeleka mtoto wetu hospitali ndipo aliposema ngoja anioneshe.SOMA ZAIDI>>